tg

Thursday, March 13, 2014

BAADHI YA WAATHIRIKA WA UKIMWI NJOMBE WAACHA KUTUMIA DAWA KWA KUDANGANYWA NA VIONGOZI WA DINI BAADA YA KUAMBIWA WATAPONYWA KWAB MAOMBI



Wadaiwa kuwaponya Kwa Maombi na Kutelekeza Dawa. Msafara wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Ukitokea Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Njombe Leo Kuelekea Saiti.
 Mwenyekiti  mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bi.Fatma Mrisho Akieleza Lengo la Tume Hiyo Kufanya Ziara Ya Siku Mbili Mkoani Njombe.


 Baadhi ya Wanafunzi Katika Shule ya Mount Living Stone Kibena Njombe.

 Hapa Baadhi ya Walimu wa Shule ya Msingi Mpechi  Njombe Wakiwa na Wajumbe wa Tume Ya Kudhibiti Ukimwi

 Tume ya Kudhibiti Ukimwi Ikizungumza na Wabafunzi Katika Shule Ya Mount Living Stone Kibena Njombe Leo



 Kamishina wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Akiwawakilisha Wakristo Askofu Mstaafu Peter Mwamasika Akizungumzia Suala la Ukimwi Njombe Leo



 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi Akikabidhiwa Taarifa ya Sheria za Kudhibiti Ukimwi Toka kwa Mwenyekiti Mtendaji wa Tume Bi.Fatma Mrisho Nje ya Ofisi za Mkoa wa Njombe.

Na Gabriel  Kilamlya Njombe.

Watu Waishio Na Virusi Vya Ukimwi Katika Mkoa Wa Njombe Wamewatuhumu Baadhi Ya Viongozi Wa Madhehebu Ya Dini Kupotosha Umma Kuwa Wanaponya Ukimwi Kwa Maombi.

Wakizungumza  Mbele Ya Mwenyekiti  Mtendaji Wa   Tume Ya Kudhibiti Ukimwi Tacaids Fatma Mrisho Baadhi Ya Watu Waishio Na Vvu Wamesema Viongozi Wa Dini Wamekuwa Wakiwalagai Waathirika Wa Ukimwi Kuwa Wanaponya Ukimwi Kwa Maombi Na Hivyo Kuacha Kutumia Dawa Na Kupunguza Makali (Arv).

Wamesema Hali Hiyo Imesababisha Baadhi Ya Waathirika  Kuacha Kutumia Dawa Na Kwenda  Kliniki Na Hivyo Kujikuta Katika Hatari Ya Kushambuliwa Zaidi Na Magonjwa Nyemelezi Ya  Ukimwi Na Hivyo Kuhatarisha Maisha Yao.

Wakiwa Kwenye Kikao Cha Wadau Mbalimbali Wa Ukimwi  Wakiwemo Wataalamu Wa Afya Katika Ukumbi Wa Halmashauriya Wilaya Ya Njombe Baadhi Ya 

Waathirika Hao Wamesema Viongozi  Hao Wa Dini   Wamekuwa Wakichangia Watu Kuacha Kutumia  Dawa Kwa Kuwadanganya Watu Kuwa Wanaponya Ukimwi Kwa Maombi.

Katika Hatua Nyingine Imegundulika Kuwa Baadhi Ya Waathirika Wamekuwa Wakiacha Kutumia Dawa Hizo Na Badala Yake Wanajiingiza Kwenye  Matumizi Ya Pombe.

Peter  Mwamasika Ni Askofu Mstaafu Wa Kanisa La Kiinjili La Kilutheri  Tanzania Dayosisi Ya Dodoma Na Kamishina Wa Tume Ya Kudhibiti Ukimwi Taifa Kwa Niaba Ya Wakristo Ambaye Amesema Kuwa Pamoja Na Viongozi Wa Dini Kupinga Matumizi Ya Kondomu Lakini Wanapaswa Kuwaelimisha Wananchi Njia Sahihi Za Kutokomeza Janga La Ukimwi.


Tume Hiyo Ilipowasili Katika Shule Ya Msingi Mpechi Ilibaini Kuwepo Kwa Upungufu Mkubwa Wa Walimu Wa Kiume Hali Iliyotajwa Kuwa Inasababisha Kushindwa

Kutolewa Kwa Elimu Ya Ukimwi Kutokana Na Usawa Wa Kijinsi,Ambapo Mmoja Wa Walimu Pekee Wa Kiume Katika Shule Hiyo Alisimama Na Kupaza Sauti Yake Akiomba Serikali Kuongeza Idadi Ya Walimu Wa Kiume Shuleni Hapo.

Kwa Upande  Wake Mwenyekiti Mtendaji Wa Tume Ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bi.Fatma Mrisho Amesema Kwa Kuwa Vijana Wamekuwa Wakikumbwa Na Janga La Ukimwi Kuliko Watu Wengine,Serikali Itaendelea Kuhakikisha Vijana Wanaelimishwa Ipasavyo Katika Masuala Ya Kujikinga Na Masuala Ya Ukimwi.

Tume  Hiyo Ya Kudhibiti Ukimwi Imeanza Ziara Ya Kuwatembelea Wananchi Mjini Njombe Kwa Siku Mbili Ambapo Pamoja Na Mambo Mengine Imewafikia Walimu Na Wanafunzi Kwenye Shule Za Msingi Mpechi Na Mount Living Stone Ambapo Hapo Kesho Inahitimisha Ziara Hiyo Ya Siku Mbili Kwa Kutembelea Shule Za Sekondari Ili Kubaini Chanzo Cha Maambukizi Hayo.

0 comments:

Post a Comment