tg

Monday, December 30, 2013

HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO YAONGOZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2013 KWA MKOA WA NJOMBE


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe Bi.Mgeni Baruan Akitangaza Wanafunzi Watakaojiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2014

 Sekretarieti ya Elimu Mkoa wa Njombe Wakati wa Kutangaza Nafasi za Kujiunga na Kidato cha Kwanza Hapo Januari Mwaka 2014.







Kupelekea Wanafunzi Kufutiwa Matokeo.




 Matokeo Hayo Yametangazwa Disemba 28 Mwaka Huu Katika Ukumbi huo Mjini Makambako


Baadhi ya Wadau wa Elimu Wakiwa Kwenye Kikao Hicho Jana Mjini Makambako Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba Akifuatiwa na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Njombe.

Habari kamili........................................................



Halmashauri ya Mji wa Makambako Mkoani Njombe Imeonekana Kuongoza Katika Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Kimkoa Ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji Njombe Kwa Mwaka 2013

Licha ya Matokeo hayo Yaliyopelekea Mkoa wa Njombe Kushika nafasi ya Tano Kitaifa Kati ya Mikoa 25 ya Tanzania Bara lakini Shule ya Msingi Kanani Iliyopo Wilayani Wanging'ombe Imefanikiwa Kutoa Mwanafunzi bora wa kwanza Kimkoa Anayejulikana kwa Jina la Neema Wihallah.

Akitangaza Matokeo Hayo Wakati wa Kuwapanga Wanafunzi hao Afisa Elimu Mkoa wa Njombe Bwana Said Nyasilo Kwa Mwaka 2013 Jumla ya Watahiniwa 18752 Wakiwemo Wavulana 8698 na Wasichana 10,967 sawa na Asilimia 59.0% Isipokuwa kwa Halmashauri ya Mji wa Makambako.

Aidha Jumla ya Wanafunzi 379 Wakiwemo Wavulana 155 na Wasichana 224 Wamekosa nafasi katika shule za Sekondari Kutokana na Upungufu wa Vyumba vya Madarasa na Uchache wa Shule Hizo.

Hata Hivyo Mwaka 2013 Jumla ya Wanafunzi 275 Wakiwemo Wavulana 170 na Wasichana 105 sawa na Asilimia 1.4% hawakufanya Mtihani Huo Ikilinganishwa na Wanafunzi 571 sawa na Asilimia 2.9% ya Mwaka 2012.

Kutokana na Hali Hiyo Mkoa wa Njombe Umewatangaza Jumla ya Wanafunzi 10984 Wakiwemo Wavulana 4884 na Wasichana 5800 Sawa na Asilimia 97% ya Wanafunzi Waliopata Alama 100 hadi 250 Wamechaguliwa Kujiunga na Masomo ya Kidato cha Kwanza Mwaka 2014.

 

Na Gabriel  Kilamlya, Makambako.

0 comments:

Post a Comment