tg

Thursday, January 3, 2013

MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE AZINDUA CHANJO MPYA ZA WATOTO LEO


 Mkuu wa wilaya ya Wanging'ombe Bi.Esterina Kilasi akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Mdandu wakati akizindua Chanjo Mpya za watoto za Nimonia na Kuhara leo.

 Kaimu Mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe Dr. Conrade Ugonile Katikati akiwa na diwani wa kata ya Mdandu Annaupendo Gombela kulia wakati wa uzinduzi wa Chanjo mpya za watoto
Wananchi wa kijiji cha Mdandu wakiwa kwenye uzinduzi wa Chanjo leo.
 Wakazi wa kijiji cha mdandu wakiwa wamekusanyika katika uzinduzi wa chanjo hizo za Nimonia na Kuhara leo.

 Mkuu wa wilaya ya Wanging'ombe akizindua chanjo za watoto kwa kuwachanja baadhi ya watoto leo huko mdandu.
Wataalamu wa afya wakiendelea na zoezi la utoaji chanjo kwa watoto mara baada ya DC kuzindua
.......................................................................................................

Zaidi ya Watoto Elfu Kumi Wenye Umri Chini ya Mwaka Mmoja wa Wilaya za

Njombe , Wanging'ombe na Halmashauri ya Mji wa Makambako Wanatarajia

Kupatiwa Chanjo ya Kuzuia Magonjwa ya Nimonia na Kuhara.

Takwimu Hizo Zimetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Bi. Esterina

Kilasi Hii Leo Wakati Akizindua Chanjo Dhidi Magonjwa ya Nimonia na

Kuhara Kwa Watoto Waliochini ya Mwaka Mmoja Katika Kijiji cha Mdandu Kwa

Wilaya za Wanging'ombe, Njombe na Halmashauri ya Makambako.

Akizungumza Kwenye Uzinduzi Huo Mkuu Huyo wa Wilaya Amewataka Wazazi na

Walezi Kuwapeleka Watoto Wao Kupatiwa Chanjo Hizo na Kuondokana na Imani

Potofu Zilizojengeka Kwa Baadhi ya Wananchi na Kwamba Chanjo Hizo

Zinalenga Kupunguza  Vifo Vya Watoto Waliochini ya Umri wa Miaka Mitano.

Kwa Upande Wake Kaimu Afisa Tarafa wa Mdandu Bwana Benson Wandelage

Amewataka Wazazi na Walezi wa Tarafa Hiyo Kuendelea Kuwapeleka Watoto Wao

Kwenye Vituo Vinavyotolea  Chanjo Hizo.

zoezi la Uzinduzi wa chanjo hizo katika halmashauri ya wilaya ya Njombe

limekuja ikiwa ni siku nne tangu halmashauri ya mji wa Njombe kuzindua

chanjo hizo katika zahanati ya Idundilanga Mjini hapa.

0 comments:

Post a Comment