tg

Saturday, February 2, 2013

SHULE YA MSINGI MADEKE NJOMBE YAKUTWA HAINA WALIMU YAONGOZWA NA VILANJA. DC AGEUKA MBOGO.

 Hawa ni miongoni mwa wanafunzi katika shule za msingi wilayani Njombe ambao wamefurahia kuongezewa walimu wa mazoezi ikiwa Shule ya msingi madeke ikiongozwa na vilanja kutokana na Utoro wa walimu.
 Mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba Akizungumza na mtandao huu mara baada ya kujionea hali ya shule hiyo ikiwa haina hata Mwalimu mmoja.
 Huyu ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi madeke ambaye amekutwa mjini Njombe akiendelea na shughuli nyingine.
Hawa ni wanafunzi wa shile mojawapo wilayani Njombe wanaopata huduma ya chakula asubuhi Uji na mchana Chakula ikiwa shule ya msingi madeke haina huduma ya chakula shuleni kwa kile kinachodaiwa wazazi hawajachanga chakula

 Katika hali isiyo ya kawaida shule ya msingi Madeke Wilayni Njombe imekutwa haina hata mwalimu mmoja na vilanja wakikabidhi kuwaongoza wanafunzi wenzao.

Hali hiyo imetokea katika shule hiyo ya madeke wakati mkuu wa wilaya ya

Njombe Bi.Sarah Dumba akifanya ziara ya kutembelea shule za wilaya ya Njombe na kisha kubaini tatizo hilo.

Aidha amese amesema alipofika shuleni hapo hakumkuta mwalimu yeyote zaidi ya mandishi yaliyoandikwa na mwalimu mkuu kuwa yeye anakwenda mjini na hivyo shule kuwakabidhi vilanja.

Kufuatia sakata hilo mkuu wa wilaya ya Njombe amewaagiza walimu kutekeleza majukumu yao na si kuendelea kuilalamikia serikali kutaka kuwatekelezea stahiki zao wakati wao hawatekelezi.Kutokana na hali hiyo mtandao huu wa www.gabrielkilamlya.blogspot.com umelazimika kumtafuata mwalimu mkuu wa shule hiyo bwana Josephat Mbugi aliyekutwa mjini Njombe kama maandishi yake yalivyoachwa shuleni hapo na kisha kukiri wazi kuwa tatizo hilo limetokana na utoro wa walimu.

Mwalimu mkuu huyo bwana Mbugi amesema kuwa hatua ya kuwaachia wanafunzi kuongoza shule hiyo imetokana na

yeye kubaki pekee yake na hivyo kujikuta akishindwa kutekeleza majukumu  yote kwa wakati mmoja na hivyo kuwakabidhi vilanja kuwaongoza wenzao.

Ameongeza kuwa  shule hiyo ina jumla walimu  wanne na wanafunzi 102  ambapo hadi sasa walimu hao wametoroka na mmoja amesimamishwa kazi kwa sababu ambazo hazikufahamika mara moja.


Kijiji cha Madeke ni miongoni mwa vijiji vilivyopo kata ya Mfiriga na kikiwa mpakani mwa mkoa wa Njombe na Morogoro huku ikitajwa kuwa walimu wanaopelekwa kufundisha shule hiyo ni wale walioshindikana katika maeneo mengine na hivyo kupelekwa kama adhabu.

Pamoja na mambo mengine lakini pia imetajwa kuwa hadi sasa wanafunzi hawapati chakula cha mchana kutokana na kile kinachodaiwa wazazi kushindwa kuchangia chakula licha ya kuchangia fedha kwa mahitaji mengine "alisema

0 comments:

Post a Comment