tg

Monday, January 7, 2013

TAARIFA YA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA NNE YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM KUANZIA MWAKA 2005 – 2012 ILIYOSOMWA NA MKUU WA MKOA MHESHIMIWA KAPT. (MSTF) ASERI MSANGI TAREHE 7 JANUARI 2013 .kikao chafanyika katika Hotel ya Agreement Mjini NJOMBE LEO.


 Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha utekelezaji wa Ilani ya Serikali kwa awamu ya NNE.

 Katibu tawala mkoa wa Njombe Bi.Mgeni Baruani Kushoto akifuatiwa na mkuu wa Mkoa wa Njombe
Capt.Mstaafu Asseri Msangi,akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Sarah Dumba mwishoni kulia ni mkuu wa wilaya ya Wanging'ombe Esterina Kilasi wakiwa kwenye kikao cha Utekelezaji wa Ilani mkoa wa Njombe.
 Mkuu wa mkoa wa Njombe akiwa na mkuu wa wilaya ya Ludewa Jumma Solomon Madaha wakiwa nje ya ukumbi wa Agreement Hotel Mara baada ya kumalizika kwa kikao leo.




 Mkuu wa mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi akitoa taarifa ya Utekelezaji wa  Ilani ya uchaguzi ccm kwa awamu ya Nne kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2012.



TAARIFA YA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA NNE YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM KUANZIA MWAKA 2005 – 2012 ILIYOSOMWA NA MKUU WA MKOA MHESHIMIWA KAPT. (MSTF) ASERI MSANGI
TAREHE 7 JANUARI 2013

Ndugu Wananchi;
Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha kuuona Mwaka Mpya wa 2013 tukiwa wazima na Afya njema.
Pili napenda kuchukua fursa hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa wananchi wa Mkoa wa Njombe pamoja na Wadau wa Maendeleo kwa kushiriki kwao kwa namna mbalimbali katika utekelezaji wa shughuli za Maendeleo na Utoaji wa huduma Mkoani kwetu.  Hotuba yangu leo inahusu Mafanikio ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha 2005 – 2012.
Ndugu Wananchi;
Katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005 na 2010, Wananchi wa Mkoa wa Njombe wamefanya shughuli mbalimbali za Kiuchumi na Kijamii.   Aidha, shughuli kuu ni pamoja na Kilimo, Ufugaji, Upasuaji wa Mbao, Uvuvi, Biashara, Ajira za Maofisini na Viwandani. Sambamba na shughuli hizi, usimamizi na ufuatiliaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa umeimarishwa ili kuhakikisha kuwa huduma kwa wananchi zinaboreshwa.   Mafanikio yaliyopatikana katika sekta mbalimbali ni kama ifuatavyo:-
1.0  UTAWALA BORA
Ndugu Wananchi;
(i) Maeneo Mapya ya Utawala
Mnamo  tarehe  1  Machi  2012  Serikali ilitangaza rasmi kuanzishwa kwa Mkoa wa Njombe ukitokea  Mkoa wa Iringa  na kutangaza katika Gazeti la Serikali Toleo Namba 9 la mwaka 2012.   Sanjari   na  kuundwa  Mkoa,  Serikali ilitangaza  kuanzishwa   kwa  Wilaya  ya Wanging’ombe  ikitokea  katika  Wilaya  ya  Njombe. Aidha, Serikali ilianzisha Halmashauri  ya  Mji  wa Njombe katika  mwaka 2007  na mwezi Julai 2012  Halmashauri ya Mji  wa Makambako ilianzishwa. 
Taratibu za kisheria zinaaendelea ili kuweza  kuanzisha  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Wanging’ombe.  Aidha, idadi ya Kata na vijiji vimeongezeka. Kuanzishwa kwa maeneo haya mapya ya utawala ni mafanikio  makubwa yenye nia ya kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi.
(ii)           Mapambano Dhidi ya Rushwa
Serikali imeendelea kufuatilia na kuhakikisha kwamba stahili zote za watumishi zinalipwa kwa wakati ili wasiingie kwenye vishawishi vya kutaka kutoa au kupokea rushwa.  Aidha, haki na stahili za utoaji huduma zimeainishwa katika mabango na mbao za matangazo ili wananchi wafahamu stahili zao. Pia elimu inaendelea kutolewa kuhusu athari za rushwa mahali pa kazi. Yote haya ni katika kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma bora na Serikali inakuwa wazi kwa wananchi wake.
(iii)           Uboreshaji wa Mishahara na stahili nyingine za Watumishi
Kwa kipindi cha mwaka 2005 – 2012, Serikali imekuwa ikiboresha mishahara na stahili mbalimbali za watumishi ikiwa ni pamoja na kuwapandisha vyeo kwa wakati, kuwajengea uwezo kwa kuwapa mafunzo na kuwawezesha kupata mikopo mbalimbali katika Taasisi za Fedha.
     (iv)  Mapambano Dhidi ya UKIMWI Sehemu za Kazi
Serikali ya Awamu ya nne imeendelea kuwahudumia watumishi wanaojitokeza kuwa wameathirika na Virusi vya UKIMWI.  Watumishi hao wanahudumiwa kwa matibabu na lishe.  Ili kufanikisha hili Serikali imetoa Waraka wa Watumishi wa Umma Na.1 mwaka 2007 ukitoa maelekezo kwa waajiri  wote kuhusu utoaji wa huduma kwa watumishi hao.
       (v)   Mpango wa Maboresho katika Sekta ya Utumishi wa Umma
Serikali imefanya maboresho ya Utumishi wa Umma kwa awamu mbili.  Katika Mpango huu mifumo mbalimbali imeboreshwa ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo watumishi wa Umma ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.  Aidha, vitendea kazi vimeweza kupatikana kupitia Mpango huu ambapo utendaji kazi katika Ofisi mbalimbali za Serikali umeimarika.
       (vi)  Vikao Mbalimbali vya Kisheria
Vikao mbalimbali vya Kisheria vimeendelea kufanyika, hili imesaidia kupunguza malalamiko kwa wananchi. Pia katika maeneo ya kazi  kuhakikisha kuwa vikao vya Watumishi na Waajiri vinafanyika mara kwa mara ili kupunguza malalamiko ya Watumishi sehemu za kazi lengo likiwa ni kuboresha huduma kwa Wananchi. Aidha, Mabaraza ya Wafanyakazi yameundwa na yanafanya kazi.
      (vii)  Kushughulikia Malalamiko Mbalimbali
Madawati ya malalamiko yameanzishwa sehemu za kazi katika Ofisi zote za Serikali ili kupokea na kushughulikia malalamiko mbalimbali yanayowasilishwa na wananchi. Sanjari na hili masanduku ya maoni yamewekwa katika sehemu za utoaji huduma ili kupata maeneo yenye udhaifu na kuyaboresha.
2.0 SEKTA YA KILIMO
Ndugu Wananchi;
Mafanikio makubwa yameonekana katika Sekta ya Kilimo na hivyo kuboresha uchumi na maisha ya Wakulima.   Maeneo yaliyoonesha ufanisi ni pamoja na:-
(i)      Wananchi wameendelea kupokea pembejeo za kilimo kwa njia ya ruzuku ambapo utaratibu huu umefanikisha upatikana wa pembejeo kwa urahisi na kuongeza tija. Katika kufanikisha mpango huu Serikali imetoa ruzuku ya pembejeo za kilimo zenye thamani ya jumla ya shilingi 36,166,982,000 hadi sasa, kiasi hicho cha fedha kimeweza kuwanufaisha wakulima kulima ekari 520,011 za mazao  ya  Mahindi  na  Mpunga.
(ii)        Uzalishaji  wa  mazao ya  Chakula  na  Biashara  umepanda  na  kufikia  tani
     1,155,45,  kwa  mwaka  2012  ikilinganishwa  na tani  463,694  mwaka 2005.
     Hii ni kutokana na kuongezeka kwa tija ya uzalishaji ambapo kwa Mahindi
     uzalishaji tija uliongezeka kutoka wastani wa tani 2 kwa hekta hadi kufikia
     wastani wa tani 3 kwa hekta, Mpunga kutoka wastani wa tani 1.5 kwa hekta
     hadi kufikia  wastani  wa  tani 2.5 kwa hekta,  Ndizi  kutoka  wastani  wa  tani
     8.5 kwa  hekta  hadi kufikia wastani wa  tani 13 kwa hekta  na  viazi mviringo
     kutoka tani 11 kwa hekta hadi kufikia wastani wa tani 15 kwa hekta.
(iii)     Kwa miaka yote saba Mkoa umeendelea kuwa na ziada ya mazao ya chakula  
    na kuwa na usalama wa Chakula Mkoani. Takwimu zinaonesha kuwa mwaka
    2011/12  Mkoa una ziada ya  tani 500,135 za nafaka na tani 222,345 za viazi
    Mviringo na Mihogo.
(iv)    Eneo  linalolimwa  limeendelea  kuongezeka  mwaka  hadi  mwaka  na  kufikia
    Ha.367,769  ambazo  ni  sawa  na  asilimia  98  ya  malengo  kwa  mazao  ya
    chakula   na  Ha. 76,971  sawa   na   asilimia   99   kwa   mazao  ya  Biashara    
    ikilinganishwa na  Ha. 232,212 za mazao ya chakula na Ha. 17,645 za mazao
    ya biashara  katika  mwaka  2005.
(v)      Skimu za umwagiliaji zilizoendelezwa/zilizoboreshwa zimeongezeka ambapo       
     mwaka  2005  kulikuwa  na  skimu 2 zilizoendelezwa na hadi kufikia mwaka
     2012 Mkoa una skimu 7 zilizoendelezwa zenye wastani wa eneo hekta 2,194
     zinazofaa kwa umwagiliaji.
(vi)      Huduma  za  ugani  zimeboreshwa  kwa  kuongeza  idadi  ya Maafisa Ugani
     ambapo mwaka  2005  walikuwa Maafisa  Ugani 172 na hadi kufikia mwaka
     2012 Mkoa una jumla ya Maafisa Ugani 363,   aidha katika vijiji ambavyo       
     havina Maafisa Ugani,  Wagani  Kazi 240 wamepewa mafunzo na kufanya 
     huduma za ugani vijijini ambapo Wagani kazi hao  hawakuwepo mwaka
     2005.
(vii)  Matumizi ya zana za kilimo yameongezeka kama inavyooneshwa kwenye
    jedwali hapa chini:-
AINA YA ZANA
IDADI  YA ZANA
MWAKA 2005
IDADI YA ZANA MWAKA 2012
ASILIMIA YA ONGEZEKO
Trekta kubwa
163
209
128.2%
Trekta za mikono (Powertillers)
0
164
100%
Plau
1,504
2,098
139.5%
Maksai
17,776
33,867
190.5%
Mkokoteni
973
1,013
104.1%
Mashine za kupandikiza Mpunga (Rice transplanters)
0
2
100%
Mashine ya kuvuna (combine harvester)
1
3
300%
3.0  SEKTA YA MIFUGO:
Ndugu Wananchi;
(i)  Idadi  ya  Mifugo  imeongezeka  katika  kipindi  cha  mwaka  2005  hadi  2012  kama
     ifuatavyo:-
AINA YA MIFUGO
IDADI  YA MIFUGO
MWAKA 2005
IDADI YA MIFUGO MWAKA 2012
Ng’ombe
151,307
171,482
Mbuzi
44,464
96,295
Kondoo
34,613
35,600
Kuku
978,564
11,896,175
Nguruwe
10,863
83,756
(ii)    Miundombinu ya Mifugo imekarabatiwa na kujengwa kama ifuatavyo:-
MAELEZO
IDADI
2005
2012
Majosho
54
82
Machinjio kubwa
3
6
Machinjio ndogo
4
10
Malambo
14
51
Mabanda ya Ngozi
4
8
(iii)    Udhibiti wa Magonjwa mbalimbali ya Mifugo kwa kutumia chanjo na uogeshaji
         umeongezeka na kufanya maambukizi ya magonjwa kupungua kama ifuatavyo:-
MAGONJWA
2005
2012
Magonjwa yaenezwayo na kupe
    80%
25%
Mdondo wa Kuku
    40%
25%
Chambavu na Kimeta
    15%
5%
Kichaa cha Mbwa
      5%
1%
Homa ya Mapafu ya Ng’ombe
      5%
0%
Minyoo (Ng’ombe, Mbuzi na Nguruwe)
     45%
15%
(iv)   Uzalishaji wa mazao ya mifugo umeongezeka kama ifuatavyo:-
MAZAO
2005
2012
Maziwa  (Lita)
1,524,312
2,202,826
Mayai
987,435
1,871,388
Jibini Kilo
8,456
13,201
Ng’ombe wanaouzwa
5,675
10,001
4.0  USIMAMIZI KATIKA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA
   Ndugu Wananchi;
(i)            Ukaguzi wa Hesabu za Halmashauri:
Kwa kipindi cha mwaka 2005 – 2011, Halmashauri zimekaguliwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na hati mbalimbali zimetolewa kama ifuatavyo:-
MWAKA
NJOMBE TC
NJOMBE DC
LUDEWA DC
MAKETE DC
2005/2006
-
Yenye mashaka
Hati safi
Hati safi
2006/2007
-
Yenye mashaka
Yenye mashaka
Hati safi
2007/2008
Hati safi
Yenye mashaka
Hati safi
Hati safi
2008/2009
Hati safi
Yenye mashaka
Hati safi
Yenye mashaka
2009/2010
Hati yenye mashaka
Yenye mashaka
Hati safi
Yenye mashaka
2010/2011
Hati safi
Hati safi
Hati yenye mashaka
Yenya mashaka
(ii)          Uboreshaji, Udhibiti na Ufuatiliaji wa Taarifa za Fedha za Umma kwenye
Halmashauri
Mkoa umepatiwa Mtaalamu Mshauri anayeshughulikia masuala ya fedha, ukaguzi na mifumo ya fedha, Mtaalamu huyo anashirikiana na Wataalam wa Sekretarieti katika kuboresha usimamizi wa fedha, ukaguzi, ufuatiliaji na utoaji wa taarifa za Matumizi ya fedha za umma kupitia utekelezaji wa Miradi mbalimbali katika Halmashauri.   Pia vitengo vya Ukaguzi wa ndani vya Halmashauri vimepatiwa magari na  Kompyuta ili  kurahisisha utendaji kazi na utoaji wa Taarifa za Ukaguzi kwa wakati.
 Mkoa una programu ya kuzijengea uwezo Halmashauri katika matumizi ya rasilimali watu na mali inayoendeshwa chini ya Programmu ya Shirika lisilo la Kiserikali la  Tunajali kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID). Programu hii inaziwezesha Halmashauri kutoa huduma kwa viwango na itasaidia kuzipatia hati safi za ukaguzi wa Hesabu ili ziweze kuendelea kufuzu kupata fedha za ruzuku za  Mamlaka za Serikali za Mitaa (Local Government Development Grant  LGDG).
(iii)          Kupeleka Madaraka kwa Wananchi:
Mkoa umesimamia kwa karibu ugatuaji wa Madaraka kwa Wananchi chini ya mfumo wa (D by D).  Mipango yote ya huduma za Kijamii na Kiuchumi kupangwa kuanzia ngazi ya Kitongoji,  Kijiji, Kata hadi ngazi ya Halmashauri, ambayo huwasilishwa ngazi ya Mkoa na baadaye Taifa. Baada ya kupitishwa mipango hiyo utekelezaji na Tathmini hufanyika katika ngazi za kijiji.  Aidha fedha za utekelezaji hupelekwa ngazi za kijiji chini ya usimamizi wa Halmashauri na Mkoa.
5.0 SEKTA YA ELIMU:
Ndugu Wananchi;
Serikali imeendelea kuboresha Elimu ya Awali, Elimu ya Msingi na Elimu ya Sekondari; ikiwa ni pamoja na elimu ya ufundi na elimu ya juu. Aidha, wananchi wameendelea kushirikishwa na kuhamasishwa katika kuandikisha watoto kwenda shule, kusimamia mahudhurio, kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia pamoja na ujenzi wa Shule za Msingi na Sekondari.
Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:-
(i)    Elimu ya Awali imepanuliwa kwa kiasi kikubwa kwani mwaka 2005 kulikuwa na wanafunzi 15,538 wa elimu ya awali na hadi kufikia mwaka 2012 kumekuwa na wanafunzi 51,767 sawa na ya ongezeko la asilimia 70%. Hii ina maana kuwa madarasa ya elimu ya awali yameongezeka kutoka madarasa 206 yaliyokuwepo mwaka 2005 hadi madarasa 365 yaliyopo mwaka 2012.
(ii)   Kiwango cha ufaulu wa Wanafunzi wa darasa la saba kimekuwa kikiongezeka   mwaka hadi mwaka. Mwaka 2005 kiwango cha ufaulu kilikuwa 63% na 2012 kiwango kimepanda na kufikia asilimia 74.5% sawa na ongezeko la asilimia 11.5%. Lengo la Mkoa ni kufikia asilimia 85% ifikapo 2015.
(iii)    Serikali  imeweka  msukumo  wa  uandikishaji  wa  wanafunzi  wenye umri wa
   miaka 7 – 13  katika  elimu  ya  msingi.    Kwa  mfano  uandikishaji   wa  watoto  
   wanaoanza  darasa  la  kwanza  umekuwa katika wastani wa asilimia 99% toka
   mwaka 2005 hadi mwaka 2012.
(iv)    Serikali  imeendelea  kujenga  na  kupanua  miundombinu ya shule za msingi
   kama vile nyumba za walimu na madarasa. Kwa mfano mwaka 2005, kulikuwa
   na  shule  za  msingi  432  na  mwaka  2012  kuna  shule 472. Kwa upande wa     
   madarasa ya  shule  za  msingi, mwaka 2005, kulikuwa na madarasa 2,340, na
   kufikia mwaka 2012,  kumekuwa  na  madarasa 3,264.   Nyumba za walimu pia
   zimeongezeka   kwa  asilimia 22.1%  yaani kutoka nyumba 1,660 zilizokuwepo
   mwaka  2005  kufikia  nyumba  2130  zilizopo  mwaka  2012.
(v)     Kwa upande wa uandikishaji wa wanafunzi wenye ulemavu, Shule Maalum za      
   Msingi zilizopo zimeendelea kuboreshwa ili kutoa huduma bora kwa Wanafunzi
   wenye ulemavu na mahitaji maalum.     Shule hizi zimeongezeka kutoka shule
   mbili zilizokuwepo mwaka 2005 hadi shule nne zilizopo sasa.
(vi)    Kwa  upande  wa shule  za  sekondari kumekuwepo  na  ongezeko la shule za
              sekondari ili kuwezesha kila kata kuwa na shule moja.    Mwaka 2005 kulikuwa
              na shule za sekondari 52 na hadi kufikia mwaka 2012, kumekuwepo na shule
              za sekondari 102. Mkoa wa Njombe una kata 96.
    (vii)   Kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza.    Mwaka
             2005  wanafunzi  walioingia  kidato  cha  kwanza  walikuwa  asilimia  63%  ya        
             wanafunzi  waliofanya  mtihani  wa kumaliza elimu ya msingi. Na mwaka 2013      
             wanafunzi  watakaoingia  kidato  cha  kwanza watakuwa asilimia 74.5 ya wale     
             waliofanya  mtihani huo.
(x)                 Mkoa  umeongeza  idadi ya wanafunzi wanaojiunga na masomo ya kidato    
  cha 5 – 6  kwa  kuongeza  idadi  ya  shule  za  kidato cha 5 – 6 kutoka shule    
  moja  iliyokuwepo mwaka 2005  hadi  shule 15  za  masomo hayo zilizopo    
  mwaka  2012.
(xi)                Nyumba za Walimu kwa shule za Sekondari zimeendelea kujengwa kutoka
             nyumba   205   zilizokuwepo    mwaka    2005    hadi  nyumba   458  zilizopo
             mwaka  2012.     Jitihada  zinafanyika  za  kufikia  lengo  la  nyumba  1,407.
(xii)         Kwa upande  wa  madarasa  ya  shule  za  sekondari  nayo  yameongezeka
 kutoka   madarasa  269  yaliyokuwepo  mwaka  2005   hadi   madarasa  990
 yaliyopo  mwaka 2012.
(xiii)       Kwa  upande  wa  Walimu  wa  shule  za  Msingi  kumekuwepo na ongezeko
 la ajira.   Mwaka  2005  kulikuwa   na   Walimu 2,709  na  mwaka 2012  kuna  
 Walimu 3,700.  Hapa  kuna  ongezeko  la Walimu 1,091 sawa na asilimia 73.
     
(xiv)       Vyuo vinavyotoa mafunzo ya ualimu pia vimeongezeka Mkoani kwani mwaka 2005 kulikuwa na chuo kimoja cha ualimu na mwaka 2012 kuna vyuo viwili vinavyotoa mafunzo hayo.
(xv)        Walimu  wa  shule  za  Sekondari  nao  wameongezeka  kwa asilimia 76, yaani kutoka  Walimu  304  waliokuwepo  mwaka  2005 hadi  Walimu 1,281  waliopo mwaka 2012
(xvi)      Kwa upande wa vyuo vikuu na vyuo vinavyotoa mafunzo ya ufundi, mwaka 2005 hapakuwepo Chuo Kikuu Mkoani, lakini kufikia mwaka 2012 Mkoa umepata matawi mawili ya kutolea elimu ya juu, na kuna vyuo vitano vya kutolea mafunzo ya ufundi.
Pamoja na mafanikio hayo, serikali mkoani inaendelea kuhamasisha jamii, watu binafsi na mashirika ya dini kuwekeza katika elimu kuanzia elimu ya awali hadi elimu ya juu na ufundi.
          
6.0.        SEKTA YA AFYA
Ndugu Wananchi;
Mafanikio yaliyopatikana katika Sekta ya Afya ni kama ifuatavyo:-
(i)                  Mwaka  2005  Mkoa  wa  Njombe  ulikuwa  na  Hospitali 10, Vituo vya Afya 19 na  Zahanati  116,  hadi  Mwaka 2012  Mkoa  una  jumla ya Hospitali 10, Vituo vya  Afya  21  na  Zahanati  152.  Hivyo   vituo  vya  kutolea  huduma vimeongezeka   kutoka  146  mwaka  2005 hadi 183 mwaka 2012 sawa na ongezeko  la  asilimia 25.3,   kama  ifuatavyo:-
1.0.         Mgawanyo wa Huduma za Afya na wamiliki Mwaka 2005.
HUDUMA ZA AFYA
MMILIKI
WILAYA
JUMLA
Njombe
Ludewa
Makete
Zahanati
1. Serikali
40
33
13
86
2. Binafsi/Shirika
17
3
10
30
    JUMLA
57
36
23
116
Vituo vya Afya
1. Serikali
3
3
3
9
2. Binafsi
6
3
1
10
    JUMLA
9
6
4
19
Hospitali
1. Serikali
1
1
1
3
2. Binafsi
3
2
2
7
    JUMLA
4
3
3
10
JUMLA
1. Serikali
44
37
17
98
JUMLA
2. Binafsi
26
9
13
48
    JUMLA
70
46
30
146
1.1.        Mgawanyo wa Huduma za Afya na Umiliki kwa Mwaka 2012:
HUDUMA ZA AFYA
MMILIKI
WILAYA
JUMLA
Njombe
Njombe TC
Makete
Ludewa
Zahanati
1. Serikali
42
22
13
39
116
2. Binafsi/Shirika
14
6
12
4
36
Vituo vya Afya
1. Serikali
4
1
3
3
11
2. Binafsi/Shirika
1
5
1
3
10
Hospitali
1. Serikali
0
1
1
1
3
2. Binafsi
2
1
2
2
7
JUMLA
1. Serikali
46
24
17
43
130
2. Binafsi
17
12
15
9
53
JUMLA YOTE
1. Serikali na Mashirika/Binafsi
63
36
32
52
183
Hivyo, Mkoa una jumla ya Hospitali 10, kati yake 3, ni za Serikali, 6 za Mashirika ya Dini na 1 ya shirika binafsi. Vipo vituo vya afya 21, kati yake 11 ni vya Serikali na 10 vya Mashirika ya Dini.  Pia tunazo Zahanati 152, Kati ya 116 za Serikali, 31 za Mashirika ya Dini na 5 watu Binafsi.
(ii)                 Katika kipindi cha mwaka 2005 na 2012, idadi ya akina Mama wajawazito wanaojifungulia katika vituo vya kutoa huduma imeongezeka. Mwaka 2005 ilikuwa asilimia 56, na Mwaka 2012 kiwango kimeongezeka na kuwa asilimia ipatayo 89.
(iii)                Kwa Mujibu wa taarifa ya Vifo vya watoto wachanga (infants Mortality rate (IMR) na watoto chini ya miaka 5 (under 5 mortality rate (U5MR), navyo vimepungua. Mwaka 2005 kulikuwa na vifo 25 kwa kila watoto 1,000 waliozaliwa hai, ambapo kwa mwaka 2012 vifo vilifikia 17 kati ya watoto 1,000 waliozaliwa hai.
(iv)         Idadi ya vifo vitokanavyo na uzazi vimepungua kutoka vifo 250 kwa kila akina mama 100,000 mwaka 2005, hadi kufikia vifo 109 kwa kila akina mama 100,000 mwaka 2012.
(v)                Aidha, kiwango cha chanjo kwa watoto wenye umri wa chini ya mwaka mmoja kimeongezeka kutoka asilimia 87 kwa Mwaka 2005 hadi kufikia Asilimia 91 kwa Mwaka wa 2012.
(vi)         Suala la ugonjwa wa UKIMWI limekuwa likishughulikiwa kwa ushirikiano na Wadau mbalimbali wakielekeza katika Kutoa Elimu ya VVU, Ushauri Nasaha na Kupima kwa hiari. Hadi mwaka 2012 kuna jumla ya Vituo vya kutolea dawa za kupunguza makali ya UKIMWI vipatavyo 36 tofauti na Mwaka 2005 ambapo kulikuwa na Vituo 6 tu.
7.0 SEKTA YA MAJI:
Ndugu Wananchi;
Katika kipindi cha awamu ya nne huduma ya maji katika Mkoa wa Njombe imeongezeka toka  54.15% mwaka 2005 hadi 61.9% mwaka 2012, sanjari na mafanikio haya ya miradi ya maji, miradi ya maji inaendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali ili kuboresha huduma kwa wananchi.
Aidha kwa kipindi hiki mifuko ya maji imefikia kiasi cha shilingi 319,695,459.59, kamati za maji 294,na vyombo huru vya watumiaji maji 13.
Hali ya huduma ya maji inategemewa kuongezeka mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa miradi ya maji  inayofadhiliwa na Benki ya Dunia kama ifuatavyo:-
Na.
WILAYA
MRADI
MFADHILI
MAELEZO
1
MAKETE
Ubiluko, Mpangala, Matamba, Mbela, Mlondwe na Ng’onde
Benki ya Dunia (WSDP)
Miradi ifuatayo inaendelea kujengwa; Ubiluko, Mpangala, Matamba ‘ Mbella,
2
LUDEWA
Ilininda, Mbwila, Lugarawa na Lumbila
Benki ya Dunia (WSDP)
 Ilininda , Mbwila ,
3
NJOMBE VIJIJINI
Masaulwa, Image, Ihang’ana, Kifumbe na Wangama
Benki ya Dunia (WSDP)
Masaulwa, Image, Ihang’ana ,
4
NJOMBE MJI
Lugenge, Kisilo, Utalingolo, Limage, Igominyi, Madobole, Njoomlole, Luponde, Magoda, Madope (Ludewa DC) na Luvuyo
Benki ya Dunia (WSDP)
 Lugenge, Kisilo, Utalingolo, Limage na Igominyi .
Aidha kwa baadhi ya miradi inayojengwa, mifumo ya uvunaji maji ya mvua itajengwa kama mfano ili wananchi waweze kjifunza na hatimaye waweze kujenga kwenye miji yao.
Utunzaji Wa Mazingira
Kuna sheria za utunzaji wa Mazingira zinazotumiwa na Vijiji ili kuhifadhi vyanzo vya maji na Mazingira kwa ujumla.  Sheria hizi ni pamoja na Sheria ya mazingira ya mwaka 2004 Na. 20 kifungu cha 57 kifungu kidogo cha 1, sambamba na Sheria ya maji Na. 11 na 12 ya mwaka 2009 zinazolinda mazingira na vyanzo vya maji.
8.0   HALI YA BARABARA
Ndugu Wananchi;
Mkoa una Barabara jumla ya Km.5, 521.26 ambazo zimegawanyika katika Halmashauri na “TANROADS”   kama ifuatavyo:-
Mji wa Njombe Km.1,248, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Km. 1,476.6, Halmashauri ya Wilaya Ludewa Km. 1,055 na Halmashauri ya Wilaya Makete Km. 619.05 na TANROADS ina jumla ya Kilomita 1,123.26.
Barabara za Lami zilikuwa hazipo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo kwa kipindi hiki jumla ya Km. 16 zimejengwa kwa mgawanyo ufuatao:-
Ludewa Km.1.5, Halmashauri ya Mji Njombe Km.2 na Makete Km.12.50 na Kilomita 2 zimeanza kujengwa katika Wilaya mpya ya Wanging’ombe.
Mnamo Mwaka wa fedha 2005/2006 – Mgao wa Mfuko wa Barabara na fedha za Maendeleo ilikuwa na Jumla ya Shilingi 2.1 Bilioni, kwa Halmashauri ya Wilaya Njombe, Makete, Ludewa na Tanroads.
Hali ya kupitika kwa barabara za vijijini imeboreshwa na kufikia hatua ya kupitika kwa asilimia zifuatazo:-
(i)      Njombe Mji toka asilimia 50 hadi 85%
(ii)    Halmashauri ya Wilaya Njombe toka asilimia 40 hadi 75%
(iii)   Halmashauri ya Wilaya Ludewa toka asilimia 35 hadi 75%
(iv)   Halmashauri ya Wilaya Makete toka asilimia 30 hadi 55%
(v)    Wakala wa barabara TANROADS toka asilimia 60 hadi 95%
Hali hii imepelekea wastani wa upitikaji wa Barabara zote za Changarawe, Udongo na Lami kuwa Asilimia 77 Ki-Mkoa.
Serikali imeendelea kuimarisha Mfuko wa Barabara “Road fund” na fedha za maendeleo ili kuongeza kasi ya Ukarabati na ujenzi wa Miundombinu. Fedha za kuhudumia Barabara zimeendelea kuongezeka ambapo Mwaka wa fedha 2012/2013 Jumla ya Shilingi 16.7 Bilioni zimepangwa kutumika Mkoani ambapo Halmashauri zimetengewa Shilingi 5.0 Bilioni na Wakala wa Barabara (TANROADS) Shilingi 11.7 Bilioni.
Nishati ya Umeme
Idadi ya wateja wanaotumia umeme kwa ujumla, katika Mkoa wa Njombe ni asilimia 18. Aidha miradi inayoendelea ya kuunganishia wateja inayofadhiliwa na REA pamoja na miradi ya TANESCO ni 65.
Miradi yote kwa ujumla tunategemea kuongeza wateja kwa asilimia 8, na hivyo kupelekea kufikia asilimia 26 mpaka 30, ifikapo Mwaka 2015, ikiwa ndio lengo la Serikali  kuhakikisha Watanzania  wanaotumia  nishati  ya  umeme  kufikia  asilimia 30. 
9.0 SEKTA YA MISITU
Ndugu Wananchi;
Sekta ya misitu imeendelea kukua kwa kipindi chote kuanzia mwaka 2005 hadi 2012. Mwaka 2005 Mkoa ulikuwa na jumla ya hekta 311,736 hadi kufikia hekta 505,990 za misitu kwa mwaka 2012. Hili ni ongezeko la asilimia 162 ambapo eneo hili ni misitu ya kupandwa na ya asili.
 Mafanikio katika sekta ya misitu ni kama ifuatavyo:-
Ongezeko la ukubwa wa eneo lililopandwa miti kutoka Hekta  137,390 kwa mwaka 2005 hadi  Hekta 207,421 kwa mwaka 2012, hii ni sawa  na ongezeko la asilimia 151
                       I.        Hifadhi ya misitu ya vijiji kutoka hekta  87,920 kwa mwaka 2005 Hadi hekta 124,025 kwa mwaka 2012 sawa na ongezeko la asilimia 141.Ongezeko hili ni kutokana na ushirikishwaji wa wananchi katika usimamizi wa misitu.
                      II.        Uvunaji wa misitu ya kupandwa kwa matumizi mbalimbali ikiwa ni pamoja na biashara ya mazao ya misitu yaani mbao umeongezeka kutoka mita za ujazo 317,874 mwaka 2005 hadi mita za ujazo 601,342 mwaka 2012 za mbao sawa na ongezeko la asilimia 189.2, nguzo kutoka mita za ujazo 1,372 mwaka 2005 hadi 3,952 mwaka 2012 sawa na ongezeko la asilimia 288.
                    III.        Mapato yatokanayo na misitu imeongezeka kutoka shilingi bilioni 254. 4 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 481.5 mwaka 2012, hili ni ongezeko la asilimi 189.3. Kwa kiasi kikubwa Mkoa wa Njombe umekuwa unazalisha mazao ya misitu kwa wingi ambayo yanatumika ndani ya Mkoa,  Mikoa mingine na Nje ya mipaka ya Tanzania. Hali hii huchangia pato la kaya Mkoa na Taifa kwa ujumla.
                   IV.         Matukio ya uchomaji moto yamepungua kutoka matukio 345 mwaka 2005 hadi 158 mwaka 2012. Hii ni kutokana na wananchi kujengewa uwezo wa kutambua na kuthamini umuhimu wa kutunza mazingira kwa kutumia sheria ndogo za vijiji na Halmashauri zilizopo.
.Kwa kutambua umuhimu wa sekta ya misitu kiuchumi na hifadhi ya mazingira, serikali imeendelea kusimamia na kuhamasisha wananchi na taasisi mbalimbali kuhusu upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa.
10.0   SEKTA YA NYUKI
Ndugu Wananchi;
Mwitikio wa Wananchi katika kutekeleza shughuli za ufugaji wa Nyuki ni mkubwa ambapo Mkoa una jumla ya mizinga 56,315 na uzalishaji wa asali na nta umeongezeka ikilinganishwa na mwaka 2005 kama ifuatavyo:-
(i)                   Uzalishaji wa asali umeongezeka kutoka lita 23,262 mwaka 2005 hadi lita 223,823 mwaka 2012 sawa na asilimia 962.
(ii)                 Uzalishaji wa nta umeongezeka kutoka kilo 690 mwaka 2005 hadi kilo 33,025.4 mwaka 2012 sawa na asilimia 4,786 kama inavyooneshwa katika jedwali lifuatalo.
Zao
Mwaka
Thamani (Shilingi)
Mwaka
Thamani (Shilingi)
Onezeko la uzalishaji %
2005
2012
Asali (lita)
23,262
58,155,000
223,823
1,678,672,500
962
Nta (Kg)
690
1,035,000
33,025.4
247,690,500
4,786
Aidha Mkoa una wajasiriamali wadogowadogo wapatao 6 ambao hujishughulisha na shughuli za kufungasha asali. Hamasa inaendelea kutolewa kwa wawekezaji ili waweze kujitokeza kuwekeza katika sekta hii muhimu kiuchumi na kimazingira.
11.0   SEKTA YA USHIRIKA:
Ndugu Wananchi;
Hali ya Vyama vya Ushirika imeendelea kuimarika hasa Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS) ambavyo vimeongezeka kutoka 52 katika mwaka 2005 hadi 90 mwaka 2012.
Aidha, Idadi ya Wanachama na Mitaji imeongezeka kutoka  wananchama 8,367 na mitaji ya Shilingi 2,694,536,767 katika mwaka 2005 na kufikia wanachama 37,719 na  mitaji ya Shilingi 17,972, 219,029 katika  mwaka huu wa 2012.
Vyama vya Mazao (AMCOS) vimeongezeka kutoka 53 mwaka 2005 na kufikia 80 mwaka 2012. Aidha, mitaji imekua kutoka Shilingi 15,194,619 na kufikia Shilingi 24,860,271. Idadi ya wanachama imeongezeka kutoka 3,484 mwaka 2005 na kufikia 7,187 mwaka 2012.
12. CHANGAMOTO NA UFUMBUZI
Ndugu Wananchi;
Pamoja na mafanikio haya makubwa niliyoyaelezea, zipo changamoto chache ambazo tunaendelea kuzipatia ufumbuzi ili kuendelea kuboresha maisha ya wananchi. Baadhi ya changamoto hizo ni kama ifuatavyo:-
·         Upatikanaji wa maji safi na salama katika baadhi ya maeneo ya Mjini (Mji wa Njombe) na baadhi ya maeneo ya vijijini (Tarafa ya Wanging’ombe).  Serikali inaendelea   kufuatilia   upatikanaji   wa   ufumbuzi   wa changamoto  hii  kwa kushirikiana  na  wadau  mbalimbali  wa  maendeleo.
·         Upatikanaji  wa  soko  la  uhakika  la  mazao  ya  kilimo  hasa  viazi mviringo na matunda.   Mkoa kwa  kushirikiana  na  Wizara ya Viwanda na Bashara imeanza kulitafutia  ufumbuzi  suala  hili  kwa  kuandaa  mpango  wa  ujenzi  wa   soko  la Kimataifa litakalojengwa katika Mji wa Makambako katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya Nne. Aidha Mkoa unaendela kuwahamasisha wakulima kuimarisha Vyama vyao vya Ushirika wa Mazao ili waweze kuwa na nguvu ya pamoja katika kupanga bei na kuuza mazao yao kwa bei nzuri.
·         Upatikanaji wa ruzuku ya pembeo za kilimo kwa zao la viazi mviringo ambalo ni chanzo   kikubwa   cha   uchumi   wa  wananchi  wa  Mkoa  wa  Njombe.   Mkoa unaendelea  kuishawishi  Wizara  husika  kufikiria  uwezekano wa kutoa ruzuku katika  zao  la  viazi.
13.  HITIMISHO:
Ndugu wananchi;
Napenda kuwahakikishia kuwa Mkoa utaendelea kusimamia shughuli za Ulinzi na Usalama ili Wananchi waweze kufanya shughuli zao za Kiuchumi na Kijamii bila kuwa na mashaka yoyote.  Wananchi wanasisitizwa waendelee kuongeza juhudi na maarifa katika shughuli za uzalishaji mali.
Aidha, ninaomba Wananchi waongeze juhudi za ujenzi wa madarasa katika shule za sekondari ili watoto wote waliofaulu darasa la saba mwaka jana (2012) waweze kuingia kidato cha kwanza katika mwaka 2013.
Ndugu Wananchi niwatakie tena Heri ya Mwaka Mpya katika mwaka 2013.
“MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU UBARIKI MKOA WETU MPYA WA NJOMBE”.

0 comments:

Post a Comment