tg

Wednesday, January 16, 2013

SIRI NZITO YAIBUKA DIWANI ALIYEFUMANIWA IRINGA , ADAIWA KUTOWEKA NYUMBANI




SIRI  nzito  imeibuka sakata la diwani wa  kata ya Ifunda jimbo la Kalenga wilaya ya  Iringa vijijini mkoani Iringa mheshimiwa  Elia Mgwila  (CCM) pichani  anayedaiwa  kufumaniwa na  mke wa mtu na kupigwa kisha kukatwa  sikio moja na kung'olewa meno matatu .

Diwani  huyo ambae  kwa siku  ya jana  mara  baada ya kutoka zahanati ya  Misheni Masumbo Ifunda kwa  matibabu  alirejeshwa nyumbani  kwake  eneo la Ifunda  Kibaoni ila hadi  sasa inasadikika amekuwa akiishi kwa  kujifungia ndani ya  nyumba yake ili kukwepa  kuonana na wapiga  kura  wake ambao  wamekuwa wakifika  kumpa  pole.

Mbali ya diwani huyo  kuchagua  maisha ya  kujificha  kwa  wapiga kura  wake  pia  inadaiwa kabla ya  kufumaniwa  diwani  huyo alionywa  vya  kutoshwa na jemba   huyo  mwenye mke kuacha kamchezo hako kabaya ka kujisogeza kwa mama  watoto  wake  ila alikana kuwa hana mahusiano na  wala hamtambui mwanamke  huyo.

Wakizungumza na  mtandao  huu  wa  www.francisgodwin.blogspot.com wasiri  wa nyeti  hiyo  wanadai  kuwa  diwani  huyo ameonywa zaidi ya mara  mbili na mmiliki halali  wa mwanamke  huyo Bw Daima Msigala ila alipuuza na kumtolea maneno ya  vitisho mwenye mke  huyo akimtaka  kuacha  kumchafulia  jina lake .

Hata  hivyo imeelezwa  kuwa diwani  huyo dowezi mara  kadhaa mkewe alifuma ujumbe mfupi katika  simu yake ya kiganjani ukitoka kwa  mwanamke  huyo mke  wa Msigala Bi Lucy Lalika wakipangana jinsi ya  kuonana na kupongezana kwa jinsi ambavyo walivyofanikiwa kusaliti ndoa  zao  kwa  kuivunja amri ya  sita ila kila alipofuatwa na kulalamikiwa  juu ya hilo aliruka futi 100 .

Jambo  lililopelekea mwenye mali Bw Msigalla  ambae ni fundi uashi kuweka mtego kwa  kudanganya  kuwa anakwenda kikazi Mafinga na ndipo  bila kufikiria mheshimiwa na mwanamke   huyo waliamua  kukutana kwa ndoa ya muda  yaani ndoa ya  usiku ndani ya chumba cha mwenye mali umbali  wa  mita kama  100 kutoka nyumbani kwa  mheshimiwa  diwani na kuamua kuivunja amri ya  sita kabla ya mwenyewe  kurejea na kutembeza kichapo na kumcharanga sikio  moja diwani huyo asiyesikia la mkuu kisha  kumtoa meno matatu na  kumweka alama ya kumcharanga mapanga  miguuni kabla ya   wananchi kufika  kumpelea kutibiwa  huku akiwa amefungwa kamba miguu na mikono kama kibaka sugu.

Wakati huo  huo  jitihada za  kumpata  diwani huyo bado zinaendelea na nyumbani kwake na nyumbani kwa mwenye chake  wote  wakiwa  wamefunga milango yao na  wapiga  kura kutoka pande zote za  kata  ya Ifunda  wakikusanyika nje ya nyumba yake  kutaka kumpa  pale  bila mafanikio.

Habari  hii  inaendelea endelea  kufuatilia mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com  utapata ukweli  wa mambo

0 comments:

Post a Comment