tg

Friday, January 18, 2013

WATUMISHI WATATU WALIOIBA FEDHA KIASI CHA TSH MILIONI 109 ZA HALMASHAURI MUFINDI ,WAREJESHA


 Bw. Limbakisye Shimwela akiwa na baadhi ya makombe ya tuzo mbalimbali za ushindi katika ofisi yake.

BAADA ya  watumishi watatu  wa idara ya uhasibu katika Halmashauri ya  wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kusimamishwa kazi kwa wizi wa  fedha za umma kiasi cha shilingi milioni 109 ,Baraza la madiwani  la  Halmashauri  hiyo  limebariki matumizi ya  fedha kiasi cha shilingi milioni 109 zilizorejeshwa kutoka kwa  watumishi hao watatu  kutumika kwa  ajili ya kutengeneza madawati ,ununuzi wa madawa katika vituo vya afya na uboreshaji wa nyumba  za  walimu.

Madiwani hayo  walitoa baraka  hizo katika  kikao  cha baraza la madiwani  kilichofanyika juzi katika  ukumbi  wa Halmashauri ya  wilaya  hiyo na kuhudhuriwa mkuu  wa wilaya ya  Mufindi Evarista Kalalu ambae alikuwa  mgeni  rasmi.


Mwenyekiti  wa Halmashauri  hiyo Peter Tweve alisema kuwa ombi ambalo  limeombwa na mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri  hiyo kwa ajili ya  fedha  hizo  zilizorejeshwa  linaungwa mkono na madiwani na kumtaka mkurugenzi kuelekeza  feddha hizo ambazo  zilikuwa ni fedha  za OC kwenda  kutumika katika shughuli hizo  za kimaendeleo .

mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Limbakisye Shimwela  aliwataja   watumishi  waliohusika na  wizi  wa  fedha  hizo na kusimamuishwa kazi kuwa ni pamoja na  Willium Fwimi ,Alan Leonard, Paulo Mwaluko  wote wakiwa ni watumishi idara ya uhasibu.

Aidha Shimwela  amewataka watumishi wote kuwa na nidhamu katika    kazi na uaminifu katika fedha, ili kufanikisha mpango wa kuleta maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.

“Hakuna kitu kizuri katika kazi kama kuwa muumini wa uadilifu, unajua unapopewa dhamana si kama wale wengine wasio na cheo kama chako hawana akili au hawana uwezo huo, bali Mungu amependa tu wewe kuwa hivyo, kwa hiyo unatakiwa kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa ili kujenga imani kwa wananchi unaowatumikia,” Alisema Shimwela.

Amesema fedha za idara ya elimu msingi shilingi Milioni 45 zitachonga madawati  600  ambayo yatagharimu shilingi Milioni 27, kwa  shule 20, huku kila shule ikipatiwa madawati 30.

  Huku shule  Milioni 18  zitakarabatiwa miundombinu ya barabara  kwa shule 6 ambazo zimekuwa kikwazo kikubwa kwa wanafunzi na walimu kufika shuleni, na kujenga nyumba ya mwalimu iliyokuwa imenguka katika shule ya msingi Nandala.

Ambapo shule za sekondari zitaboreshewa maabara 8 (Mobil Laboratories) zitakazogharimu jumla ya shilingi Milioni 48 ili kuwawezesa wanafunzi wa masomo ya Sayansi kufanya vizuri kwa kupatiwa mafunzo kwa vitendo.

Na milioni 7 ikikamilisha Bweni la wanafunzi wa sekondari ya Ilogombe na Milioni 8 zikipelekwa katika idara ya afya na hivyo gharama ya shughuli hizo kukamilisha jumla ya  shilingi Milioni 109 ya fedha zote ambazo zilikuwa zimeibwa.

Hata hivyo wananchi wameupongeza uongozi wa Halmashauri hiyo,   ukiongozwa na kusimamiwa na Mkurugenzi wake Bw. Limbakisye Shimwela kwa kufanikisha fedha hizo kurejeshwa na hivyo kuchangia shughuli za maendeleo na uchumi.

 Wizi huo wa kitaalamu uliofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa  taasisi ya kifedha hapa nchini (NMB) ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, kwa kushirikiana na baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, na kuchepusha  fedha za Halmashauri hiyo zaidi ya Shilingi Milioni 109 kwa manufaa yao binafsi.

Wakizungumzia sakata hilo katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, kilichokaa kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo, pamoja na wizi wa fedha hizo, ambapo Madiwani walisema licha ya watumishi hao kurudisha fedha hizo lakini taratibu za kisheria zinapashwa zichukuliwe dhidi yao ili iwe fundisho kwa wengine.

Akichangia hoja ya fedha hizo za Umma, Evaristo Luhunga diwani wa Kata ya Ikweha alisema watumishi hao wanatakiwa kupewa adhabu licha ya kurejesha fedha hizo, kwani wamechangai kudumaza uchumi wa Halmashauri na wananchi wake.

“Hatua hii tuliyofikia inadhihirisha wazi juu ya kazi kubwa tulioyoifanya katika kufuatilia fedha hizi, lakini nisingependa tuishie hapa, kwani   watumishi wengi wamekuwa wakicheza na fedha za umma, lakini nini madhara ya wizi wa fedha hizi za wananchi, kuna haja ya kuwachukulia hatua za kisheria, ili iwe fundisho kwa watumishi wengine wenye tabia kama hizi,” Alisema Luhunga.

Naye Ernei Nyeho diwani wa Kata ya Mdabulo amesema inapotokea fedha zilizopitishwa na baraza la madiwani kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali halafu watu wachahe kwa maslahi yao binafsi wanachukua, watu hao wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

“Mimi katika Kata yangu fedha hizi zililenga kuboresha mradi wa elimu na afya kwa kununua madawati pamoja na kujenga madarasa, lakini siyo tu kwenye kata yangu, tatizo hili limeyumbisha uchumi wa Halmashauri nzima,” Alisema Nyeho.

0 comments:

Post a Comment