tg

Friday, January 24, 2014

NDOTO ZA KUANZA KWA SHULE YA MSINGI RUHUJI "B"NJOMBE ZAYEYUKA.


Mwenyekiti wa wafanyabiashara kamati ujenzi wa madarasa shule ya msingi Ruhuji bwana Zephania Msigwa kulia akiwa na makamu wake bwana Solanus Mhagama wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wakiweka mikakati ya uchangishaji michango Ya Shule Hiyo.

 Shule ya Msingi Ruhuji B Iliyopo Katika Halmashauri ya Mji wa Njombe Imeshindwa Kuanza Muhula wa Masomo Kwa Mwaka Huu Kama Ilivyokuwa Imetarajiwa Kutokana na Shule Hiyo Kutokamilika .

Akiongea na Uplands Redio Afisa Elimu Shule ya Msingi  Halmashauri ya Mji wa Njombe Zegeli Shengeli Amesema Shule Hiyo Ambayo ni Mpya Haiwezi Kuanza Muhula wa Masomo Kwa Sasa Kutokana na Mapungufu Yaliyopo Katika Shule Hiyo na Kuongeza Kuwa Ili Shule Hiyo Ifunguliwe Kunahitajika Vyumba Vitatu na Ofisi za Walimu.

Afisa Elimu Huyo Amesema Licha ya Jitihada za Wananchi na Wadau wa Elimu Kukamilisha Ujenzi wa Vyumba Vinne Kwa Ajili ya Madarasa Pamoja na Vyoo Lakini Wananchi Hao Wanatakiwa Kuongeza Vyumba Viwili na ofisi za

Walimu Ili Kukidhi Mahitaji Shuleni Hapo.

Wananchini Mjini Njombe Kwa Kushirikiana na Wafanyabiashara Walianzisha  Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi Ruhuji B Kwa Lengo la  Kutaka Kupunguza Msongamano wa Wanafunzi Uliopo Katika Shule ya Msingi Ruhuji.

Shule Mpya ya Msingi Ruhuji B Ilitarajiwa Kuanza Kupokea Wanafunzi wa Muhula wa Masomo Mwaka Huu Lakini Hadi Sasa Imeshindwa Kufanya Hivyo.


Kwa Kushindwa Kufunguliwa Kwa Shule Hiyo Katika Kipindi cha Mwaka Huu Kunawafanya Wazazi na Wananchi Kufanya Kazi ya Ziada ya Kuanza Kuchangia Upya Michango Mingine

0 comments:

Post a Comment