tg

Tuesday, January 28, 2014

BAJETI NDOGO NI KIKWAZO KWA MAENDELEO YA KATA-MAKAMBAKO NJOMBE.

Pichani ni diwani wa kata ya Mjimwema Makambako Bwana Alimwimike Sahwi Akizungumza na Mtandao Huu.
Na Gabriel  Kilamlya Makambako
 
Halmashauri ya Mji wa Makambako Imeshauriwa Kutenga Bajeti Kulingana na Uhitaji na Idadi ya Watu Katika Kata za Halmashauri Hiyo Ili Kufanikisha Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Kwa Kata za Halmashauri Hiyo.

Rai Hiyo Imetolewa na Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Halmashauri Hiyo Wakati Wakiongea na gabrielkilamlya.blogspot.com na Kusema Kuwa  Baadhi ya Kata ni Kubwa na Wingi wa Watu Hivyo Bajeti Zinazotengwa Kwa Kata Hizo Hazitoshelezi Kutekeleza Miradi ya Maendeleo Ikilinganishwa na Kata Nyingine Ambazo Zina Idadi Ndogo ya Watu na Maeneo Madogo.

Miongoni Mwa Wajumbe Waliotoa Rai Hiyo ni Diwani wa Kata ya Mjimwema-Makambako Alimwimike Sahwi Ambaye Ameeleza Kuwa Kata Yake Inakabiliwa Changamoto ya

Bajeti Ndogo Ikilinganishwa na Idada ya Watu na Ukubwa wa Kata ya Mjimwema Hali Inayosababisha Huduma za Kijamii Zinazotolewa Katika Kata Hiyo Kuwa Chini ya Kiwango.

Aidha Diwani Sahwi  Amependekeza Kugawanywa Kwa  Kata ya Mjimwema na Kuwa Kata Mbili Ili Kusogeza Huduma za Kiutawala na Kijamii Karibu na Wananchi Kutokana  na Kata Hiyo Kuwa na Idadi Kubwa ya Watu Pamoja na Eneo Kubwa Kiutawala.

Hata Hivyo Diwani Sahwi Ameipongeza Serikali Kwa Kuipa Kipaumbele Kata Hiyo Katika

Mradi wa Ujenzi wa Barabara Zilizomo Ndani ya Kata ya Mjimwema
Ambapo Takribani Kilomita 49 Zitatengenezwa na Kwamba Tayari Wakandarasi Wamesaini

Mikataba ya Ujenzi wa Barabara Hizo.

0 comments:

Post a Comment