tg

Saturday, July 20, 2013

NDUGU WATATU WAGONGANA NA MMOJA AFARIKI PAPO HAPO WILAYANI WANGING'OMBE NJOMBE LEO.

>...Majeruhi wawili wakmibizwa Hospitali ya Ikonda Makete.
 
 Hiyo ndiyo Baiskeli iliyokuwa ikitumiwa na Marehemu kabla ya Mauti Kumkuta.
 Hii ndio Pikipiki iliyosababisha Ajali Mbaya Leo ya Mwendesha Baiskeli na Kusababisha Kifo Papo hapo.

 Hii ndio Barabara inayotumiwa kwa Kasi Kubwa baada ya Kulimwa na Hivyo Kusababisha Ajali za Mara kwa Mara Wilayani Wanging'ombe.

 Mwili wa Marehemu Linus Nziku mkazi wa Mdasi Wanging'ombe ukiwa Umefunikwa na Kuondolewa Katikati ya
Barabara alipogongwa.
 Mwendesha Baiskeli Marehemu Linus Nziku[45] aliyegongwa na Kufariki Papo hapo leo Asubuhi Katika Eneo la Nyaugao Mpakani Mwa Kijiji cha Makoga na Mdasi.


 Kona Iliyosababisha Ajali ya Mmoja Kufariki na Wengine Wawili Kujeruhiwa Vibaya na Kukimbizwa Katika Hospitali ya Ikonda Makete leo Asubuhi Huko Mdasi Wanging'ombe.
 Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Gerson Lwenge akiwasili eneo la Tukio Hilo ambako alitakiwa Kufanya Mkutano na Wapiga Kura wake na Kisha Kulazimika kuahirisha Mkutano Huo.
 Hapa Mbunge Lwenge akitoa Pole katika Msiba Huo na rambi rambi ya Tshs.Laki Moja Barabarani Ulipotokea Msiba kabla ya Jeshi la Polisi Kuwasili Eneo Hilo.

Na Gabriel Kilamlya.

Mtu Mmoja Amefariki Dunia na Wengine Wawili Wamejeruhiwa Katika Ajali ya Pikipiki Iliotokea Leo Asubuhi Katika Kijiji Cha Mdasi Kata ya Makoga Wilayani Wanging'ombe Mkoani Njombe.

Wakizungumza na Kituo Hiki Baadhi ya Mashuhuda wa Ajali Hiyo Akiwemo Diwani wa Kata ya Makoga Bw Abraham Chaula Amesema Ajali Hiyo Imetokea Leo Katika Barabara Kuu ya Njombe - Makete.

Amemtaja Mtu Aliefariki Kwenye Ajali Hiyo Kuwa ni Linus Nziku Mkazi wa Kijiji Cha Mdasi na Kusema Kuwa Majeruhi Wawili Wamekimbizwa Katika hospitali ya Ikonda Kwa Matibabu Zaidi.

Aidha Pamoja na Kuelezea Mazingira ya Tukio Hilo,Bw Chaula Amewashauri Watumiaji wa Vyombo Vya Usafiri Hasa Pikipiki Kuwa Makini Wanapokuwa Barabarani.

Jeshi la Polisi Limethibitisha Kutokea Kwa Tukio Hilo.
................................................................................................

0 comments:

Post a Comment