tg

Saturday, July 20, 2013

MADIWANI WALIA NA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

Mkuu wa wilaya ya makete bi Josephine Matiro

Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya makete wamelalamikia utendaji mbovu wa watendaji  wa vijiji na kata ambapo zaidi ya watendaji ishirini waliopo  katika kata ishirini na mbili  wamedaiwa kujihusisha na unywaji pombe hali inayopelekea kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Wakitaja majina ya watendaji  na hali  utendaji wao wa kazi  madiwani  katika kikao cha robo ya nne  ya mwaka 2012/2013   wamasema kuwa pamoja na upungufu  wa watumishi   hao   lakini waliopo wana matatizo mbalimbali  yakiwemo ulevi na utoro wa kuto kukaa katika vituo vyao vya kazi hadi kusababisha kushindwa kukusanya mapato na kuiingizia hasara  halmashauri hiyo.

Pia katika baraza hilo wakiendelea kutoa malalamiko hayo wamesema kuwa katika kata zao kuna upungufu wa watumishi hao ishirini na moja  na watumishi wengine waliopungufu ni maafisa mifugo na  kilimo.


kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Makete Bw Idd Nganya amekiri kuwepo kwa upungufu huo  na kusema kuwa  uuondoshwaji wa watumishi hao bila taarifa katika sehemu zao za kazi bila taarifa kwa baadhi ya viongozi  wakiwemo madiwani katika kata zao

Pia mkurugenzi mtendaji huyo  amewataka madiwani hao  kuacha tabia ya kuwakataa baadhi ya viongozi  wakiwemo wanaohamishwa kutokana na matatizo wanayokutwa nayo katika  vituo vyao vya awali.

Aidha Baraza hilo lililoishia hapo jana   limepitisha waraka wa kuwafukuza kazi watumishi nane wa sekta mbalimbali wakiongozwa na wauuguzi  na maafisa ugani kutokana na tatizo la utoro wa muda mrefu

Baraza hilo pia limemchagua Aliyekuwa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri Jison John mbalizi kuendelea kushikiria wadhifa huo sambamba na uchaguzi wa kamati mbili na wenyeviti wao.

0 comments:

Post a Comment