tg

Wednesday, February 19, 2014

DC MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI WA MANUNUZI HEWA YA MIL.14


 huyu ndiye bw Evagrey Keiya Anayeshitakiwa kwa kosa la kufanya manunuzi hewa pamoja na mhasibu wake enzi akikaimu nafasi ya DAS. picha na maktaba


Na James Festo,Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Esterina Kilasi hapo jana  ametolea ushahidi  mbele ya mahakama ya Wilaya ya Njombe dhidi ya kesi ya manunuzi hewa wa magurudumu matano na betri mbili za gari vyoti vikiwa na thamani ya shilingi milioni 14 inayomkabili aliyekuwa kaimu katibu tawala wa wilaya hiyo ya wanging'ombe bw evegray keiya.


Akitoa ushahidi wake mahakamani hapo , mkuu huyo wa Wilaya ya Wanging'ombe ambaye ni shahidi namba moja ameiambia mahakama kuwa ofisi yake  pamoja na aliyekuwa akikaimu ofisi ya  katibu tawala  Wilaya ya Wanging'ombe  waliagiziwa  magurudumu tano aina ya gunrub kwa ajili ya gari yake lakini hakuwahi kuyaona  magurudumu hayo  katika ofisi yake .

kwa kipindi kile yanaletwa magurudumu hayo nilikuwa natumia gari niliyopewa na  Halmashauri ya Wilaya Njombe  kwa kipindi hicho sikuwa na  umuhimu wa magurudumu hayo lakini baada ya miezi mitatu baadae nilipotaka kubadili magurudumu sikuyaona........alisema Bi Kilasi

Akitoa ushahidio mahakamani hapo shahidi namba mbili ambaye ni afisa manunuzi wa Mkoa wa Njombe  Gaitan  Malio Lugenge  aliiambai mahakama kuwa alipokea taarifa ya ununuzi wa magurudumu matano na betri mbili aina ya n70 na kusema kuwa betri moja liliwekwa kwenye gari lenye namba za usajili stj 6821 ya katibu tawala Mkoa wa Njombe .

Akiendelae kutoa ushahidi mahakamani hapo shahidi namba mbili Gaitan  Malio Lugenge
Ameieleza mahakama kuwa magurudumu waliyoyapokea yalikuwa tofauti na yale yaliyoagizwa yanunuliwe kwani magurudumu waliyoyapokea yalikuwa ni bridgestoni badala ya gunrub.

Kwa upande wao washtakaiwa wakitetewa wakili wao hawakutakiwa kujibu chochote

Mara baada kusikiliza utetezi wa upande wa mashtaka hakimu wa mahakama hiyo John kapokolo ameahirisha kesi hiyo hadi machi tano mwaka huu itakapo sikilizwa tena mahakamani hapo na washitakiwa wameachiwa kwa dhamana.

Na katika   kesi  nyingine Anna Wiketye (33) mkazi wa  mtaa wa bomani   kwenye halmashauri ya mji njombe ambaye pia ni afisa tawala wa Wilaya Njombe  amefikishwa mahakamani hapo ili kujibu shtaka linalo mkabili  ambapo inadaiwakuwa alitoa ushahidi wa uongo kinyume na kifungu cha sheria namba 102 sura ya kwanza na kifungu namba 104 sura ya 16 cha sheria zas kanuni za makosa ya adhabu katika kesi inayomkabili  aliyekuwa katibu tawala wa halmashauri ya wilaya ya njombe.

Akisoma hati ya mashtaka mwendesha mashtaka wa serikali bw Riziki  Matitu alisema kuwa mnamo novemba 18 mwakajana mshtakiwa alifikishwa mahakamani hapo ili kutolea ushahidi wa kesi ya .Bori Salonge Ally, Evegray  Keiya na  Ibrahim Konga   na kutoa ushahidi wa uongo ulioufanya upande wa  mashitaka kumuondoa katika orodha  ya mashahidi  kwenye kesi ya matumizi mabaya ya ofisi  na kusababisha hasara ya shilingi milioni mbili za  Halmashauri hiyo.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitoa ushahidi ambao unakinzana na ushahidi  aliowahi kutoa alipokuwa akihojiwa na taasisi ya kupambana na rushwa  ushahidi unaosema kuwa alitoa kibali cha mafuta ya  mafuta ya gari  binafsi kwa matumizi ya ofisi badala yake mafuta hayo yalitumiwa kwa matumizi binafsi.

Kwa upande wake mshitakiwa akijibu mashtaka yanayomkabili amekubali kutoa maelezo hao kwa maofisa wa takukuru  na kusema kuwa ushahidi huo aliutoa  kutokana na mazingira aliyokuwa nayo wakati akihojiwa katika ofisi hizo na haukuwa hiari yake.

Katika kuhakikisha  haki inapatikana  mahakamani upande wa jamhuli  umenuia kuwaita mashahidi watatu ambao ni Rehema  Mpagama,Roda Lupondo na Lukas Sweve huku vielelezo vikiwa ni  hati ya maelezo  kutoka takukuru.

Hata hivyo hakimu wa mahakama hiyo  ameiahirisha kesi hiyo hadi tarehe tano  mwezi wa tatu mwaka huu na mshitakiwa yuko nje kwa dhamana.   

0 comments:

Post a Comment