Askari wa Kike wakifanya Maonesho wakati wa Kuhitimu Mafunzo yao ya Awali Mjini Moshi Leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani Dk.Emmanuel Nchimbi akifunga Mafunzo ya Awali ya CCP MJINI MOSHI Leo
Zaidi ya Askari Polisi Mia Mbili wanatarajiwa Kuwasili Kikazi Mkoani NJOMBE Mara baada ya Kuhitimu Mafunzo yao Moshi Kilimanjaro Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe ACP Fulgency Ngonyani Amesema Askari hao watasaidia Katika Suala la Ulinzi na Usalama wa Mali za Raia na Watu Wenyewe Mkoani Njombe Wakiwemo wafanyabiashara Wanaopatwa na Matukio ya Ujambazi na Mali zao.Akizungumza na Wafanyabiashara ambao ni Wanachama wa NMB BUSINESS CLUB Mkoa wa Njombe Hivi Karibuni Kamanda Ngonyani alisema Askari Hao watasaidia Kupunguza adha na Kudhibiti Matukio yanayoendelea Kushika Kasi Mkoani Hapa.Jumla ya Askari Polisi 3092 Wamehitimu Mafunzo yao ya Awali Huko Moshi ambao Hivi karibuni wanaingia Mitaani Kupambana na Wahalifu.
0 comments:
Post a Comment